Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula watoa tamko

0
910

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula Nchini -NFRA, Vumilia Zikankuba amesema kamwe hatanunua mahindi ya wakulima yasiyo na ubora.

Zikankuba ametoa kauli hiyo mbele ya Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mathew Mtigumwe ambaye amekutana na wakulima wa Mkoa wa Katavi ambao  wanalalamika kuwa mahindi yao hayajanunuliwa kutokana na kukosa ubora.

Jumla ya Tani 2500 za mahindi za wakulima zimeshindwa kununuliwa kutokana na madai ya mahindi yao kukosa ubora unaotakiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini.