Wahandisi wazembe kutopewa kazi za miradi ya maji nchini

0
1048


Serikali imesema haitawajumuisha baadhi ya wahandisi wanaozembea kukamilisha miradi mbalimbali ya maji katika Wakala wa Maji Vijijini na Mijini mara wakala huo utakapoanza.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso katika siku ya kwanza ya ziara yake Mkoani Kagera ambapo amekagua mradi wa maji wa Manispaa ya Bukoba ambao umefadhiliwa na Benki ya Dunia kwa zaidi ya Shilingi bilioni thelathini na nane.

Japokuwa mradi huo uliogharimu zaidi ya Shilingi bilioni thelathini na nane kwa ufadhili wa Benki ya Dunia bado haujaweza kukidhi mahitaji ya maeneo yote.

Meya  manispaa Bukoba , Chifu Kalumuna akaipongeza serikali kwa hatua kubwa ya kupunguza adha ya upatikanaji wa maji katika mji huo.

Kisha Naibu Waziri wa Maji Jumaa aweso pamoja na kupongeza ufanisi katika mradi huo bado anaonekana kutoridhika katika ujenzi wa miradi mingine ya maji Mkoani Kagera akitolea mfano mradi wa Katoke Wilayani Muleba.