Wahandisi wa Maji Ruvuma na Mbeya wasimamishwa kazi

0
1114

Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Maji kumsimamisha kazi mara Mhandisi wa Maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Vijijini, Vivian Mdolwa kwa tuhuma za ubadhilifu wa miradi ya maji aliyoifanya akiwa Mhandisi wa Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma.

Naibu Waziri Aweso pia amemsimamisha kazi Mhandisi wa Maji wa Mkoa wa Ruvuma, Genes kimaro kwa kushindwa kusimamia miradi hiyo ya maji na kusababisha wananchi kuendelea kupata shida ya huduma ya maji.

Wananchi wa Kata ya Litumbandyosi Wilaya ya Mbinga  wamekosa  maji kwa muda mrefu  licha ya miradi ya maji mitatu katika kata hiyo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 840 kukamilika.