Wafugaji mkoani Katavi wamaliza mgogoro na wakulima

0
1007

Baadhi ya wafugaji mkoani Katavi wameanza kutekeleza mpango wa kumaliza migogoro baina yao na wakulima kwa kupanda nyasi kama malisho ya mifugo yao.

Afisa Mifugo wa mkoa wa Katavi, Zediheri Mhando amesema tayari serikali mkoani humo, kupitia sheria ya matumizi bora ya ardhi wametenga hekta zaidi ya laki moja ambayo wafugaji wamepatiwa bure maeneo ili kuendelea na upandaji wa malisho ya wafugaji hao.

Ameongeza kuwa zoezi la upandaji wa malisho katika kijiji cha Kapanga litaondoa migogoro baina yao na kwamba sheria ya matumizi bora ya ardhi imezingatiwa.