Wadau wa afya wakutana Dar es salaam

0
1594

Chuo Kikuu cha Aga Khan kina mpango wa kuandaa mapendekezo yatakayowasilishwa kwenye mamlaka husika ili kusaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto katika maeneo mbalimbali nchini.

Hayo yamebainika jijini Dar es salaam wakati wa mkutano ulioshirikisha wadau mbalimbali wa afya ya uzazi, mkutano uliokua na lengo la kuandaa mapendekezo hayo.

Akizungumza kando ya mkutano huo, Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan Dkt Lucy Hwai ameiomba serikali kuhakikisha madaktari bingwa wa masuala ya uzazi wanapelekwa katika maeneo ya vijijini ambako kuna vifo vingi vya mama na mtoto ili kusaidia kupunguza vifo hivyo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa afya ya uzazi na mtoto kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,  -Makuwami Mohamed amesema kuwa ushirikiano baina ya sekta binafsi na serikali ni muhimu katika kupunguza vifo hivyo vya mama na mtoto.