Vitabu vya kiada kuendelea kuchapishwa na kusambazwa

0
2200

Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole-Nasha amesema kuwa serikali imejipanga kuchapisha na kusambaza vitabu zaidi ya Milioni Kumi vya kiada kwa shule za msingi nchini ikiwa ni jitihada za kutatua changamoto ya upungufu wa vitabu hivyo.

Akijibu swali bungeni jijini Dodoma, Naibu Waziri Ole-Nasha amesema kuwa tayari serikali imechapisha na kusambaza vitabu Milioni Kumi vya darasa la Kwanza hadi la Tatu na vitabu Elfu Nne vya darasa la Nne.

Naye Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt Hussein Mwinyi ameliambia Bunge kuwa katika kukabiliana na changamoto ya idadi ndogo ya vijana wanaojiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa, serikali imejenga kambi mpya ya mafunzo itakayochukua idadi kubwa ya vijana ikilinganisha na siku za nyuma.

Bunge linaendelea na mkutano wake wa Kumi na Mbili jijini Dodoma.