Viongozi wa polisi matatani

0
1986

Rais John Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kagera, – Augustine Ollomi, Kamanda wa polisi wa wilaya ya Kyerwa, – Justine Joseph, mkuu wa upelelezi wa wilaya ya Kyerwa, – Everist Kivuyo na mkuu wa kituo cha polisi cha Kyerwa, – Robert Marwa ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za kuhusika katika magendo ya zao la kahawa katika wilaya ya Kyerwa pamoja na tuhuma nyingine.

Rais Magufuli pia amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Jacob Kingu na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Simon Sirro kuhakikisha uchunguzi wa kina unafanyika na hatua stahiki zinachukuliwa endapo watabainika kuhusika katika magendo ya kahawa na makosa mengine kwa mujibu wa sheria.

Tuhuma dhidi ya viongozi hao wa polisi katika wilaya ya Kyerwa zimebainika wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wilayani humo.