Vijana wanaoishi kambi ya Nunge watakiwa kuondoka

0
2862

Vijana wanaoishi katika kambi ya kulea wazee wasiojiweza ya Nunge wilayani Kigamboni jijini Dar Es Salaam wametakiwa kuondoka kwenye kambi hiyo ifikapo kesho kwa kutokuwa na sifa ya kuendelea kuishi hapo.

Akizungumza kambini hapo Mkuu wa wilaya ya Kigamboni, Sara Msafiri amesema wameamua kuwaondoa kutokana na agizo la serikali lililowataka kuondoka tangu mwezi Januari mwaka 2016 lakini hadi sasa vijana hao bado wanaendelea kuishi kambini hapo.

Vijana wapato 34 ambao ni yatima waliokuwa wanaishi kambini hapo walichukuliwa kutoka kwenye makao ya taifa ya watoto Kurasini baada ya kupilitiza umri wa utoto.