Utafiti wabainisha Malaria yapungua nchini

0
1948

Utafiti wa viashiria vya ugonjwa wa Malaria kwa mwaka 2017 unaonyesha kupungua kwa maambukizi ya ugonjwa huo nchini kutoka asilimia 14 ya mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 7.3.

Akiwasilisha matokeo ya utafiti huo jijini Dar Es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa amesema utafiti huo umefanyika nchi nzima.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka maafisa afya na mazingira katika halmashauri zote nchini kujikita katika usafi wa mazingira ili kuua mazalia ya mbu wanaosababisha malaria.

Utafiti wa viashiria vya Malaria wa mwaka 2017 nchini umefanyika ili kutoa taarifa zitakazosaidia kufuatiliaย  hali ya malaria nchini.