Upotevu wa dawa wamkera Naibu waziri

0
2147

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile ameiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Nachingea mkoani Lindi, Mganga Mkuu wa Mkoa pamoja na wa wilaya kufanya uhakiki wa dawa katika hospitali ya wilaya ya Nachingwea.

Dkt Ndugulile ametoa agizo hilo baada ya kutembelea hospitali hiyo na kubaini mapungufu katika usimamizi wa dawa na kusababisha dawa nyingi kupotea.

Amesema kuwa changamoto ya upotevu wa dawa si kwa wilaya ya Nachingwea pekee, bali ni kwa wilaya nyingi zilizopo maeneo ya pembezoni.

Akisoma taarifa yake kwa Dkt Ndugulile, Mkuu wa wilaya ya Nachingwea, -Rukia Muwango amesema kuwa tayari wilaya hiyo imepokea fedha kwa ajili maboresho ya vituo vya afya na hospitali ya wilaya.

Akiwa katika wilaya hiyo ya Nachingwea, Naibu Waziri huyo wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amehitimisha kampeni ya upimaji wa virusi vya Ukimwi kwa ngazi ya wilaya na kutumia nafasi hiyo kuagiza mikoa na wilaya ambazo bado hazijafanya kampeni hiyo kufanya mara moja.