Unywaji wa pombe uliokithiri chanzo familia kutelekezwa

0
1194

Unywaji wa pombe uliokithiri mkoani Kigoma umechangia kuongezeka kwa idadi ya wanaume wanaotelekeza familia zao na hivyo kusababisha ongezeko la watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.

Baadhi ya wanawake waliotelekezwa na wenzi wao katika kijiji cha Mabamba wilayani Kibondo wameiomba serikali kuwasaidia ili wapate haki ya matunzo ya watoto wao.

Wakizungumza katika mdahalo wa kuielimisha jamii kuhusu athari za ukatili wa kijinsia,baadhi ya wanawake waliotelekezwa na wenzi wao katika wilaya ya Kibondo wameiomba serikali kuwasaidia kupata haki ya matunzo ya watoto wao.

Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma inakabiliwa na ongezeko la watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kutokana na baadhi ya wazazi wa kiume kutelekeza familia zao.

Hali hiyo imechangia baadhi ya watoto kukimbilia mitaani kwa  kukosa mahitaji muhimu.