Ujio wa ndege mpya kuchochea thamani za bidhaa nchini

0
846

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela amesema ujio wa Ndege aina ya Airbus 220-300 ya Shirika la Ndege nchini -Atcl utaongeza mnyonyoro wa thamani wa bidhaa zinazozalishwa katika sekta mbalimbali hapa nchini.


Mongela ameyasema hayo Jijini Mwamza wakati ndege hiyo ilipoanza safari zake rasmi hapa nchini kwa kusafiri kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza na kusema kuwa ndege hiyo itachochea uchumi na ajira kwa watanzania.
 

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula amesema miundombinu ndio njia kuu katika kuutangaza utalii na kukuza uchumi wa nchi.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Mawasiliano Atcl, Josephat Kangirwa amesema kuwa ndege hiyo pia itafanya safari za kwenda India, China na Thailand.