Uhakiki wachelewesha nyongeza ya mishahara

0
2340

Serikali imesema inatambua kuwa wafanyakazi wanahitaji nyongeza ya mishahara lakini zoezi hilo limekwama kutokana na zoezi la uhakiki la mwaka 2016/17 na kwamba kwa sasa wafanyakazi wanaingizwa kwenye kanzi data baada ya uhakiki.

Akijibu swali bungeni mjini Dodoma Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde amesema nyongeza ya mishahara itafanyika baada ya zoezi la kanzi data kukamilika.

Katika hatua nyingine Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama ameliambia Bunge kwamba serikali imekuwa ikitenga shilingi bilioni kumi na tano kwa ajili ya kufanya tafiti na kutoa ujuzi kwa wananchi ili kufanikiwa katika ujenzi wa viwanda.