Tume ya Utumishi wa Umma yapata viongozi

0
1586

Rais John Magufuli amemteua Jaji Mstaafu Steven Bwana kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma kwa kipindi cha miaka mitatu.

Pamoja na kumteua Mwenyekiti wa Tume, Rais Magufuli pia amewateua Makamishna watano wa Tume ya Utumishi wa Umma.

Walioteuliwa ni
George Yambesi, Balozi Mstaafu John Haule, Immaculate Ngwale, Yahaya Mbila na Balozi Mstaafu Daniel Ole Njoolay.

Uteuzi huo wa Mwenyekiti na Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma umeanza Novemba 22 mwaka huu.