Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imesema, mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini ni za masika.
Akizungumza katika mahojiano na TBC, Mtaalam na Mchambuzi wa hali ya hewa kutoka TMA Rose Senyagwa amesema, mvua hizo zitaendelea kunyesha katika maeneo mengi nchini.
Amewataka Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari, ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na mvua hizo