TANZIA: Mwanasheria mkongwe Dkt. Lamwai afariki Dunia

0
258

Mwanasiasa na Mwanasheria mkongwe nchini Tanzania, Dkt. Masumbuko Lwamai amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Mei 05, 2020.

Dkt. Lwamai alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Tumaini.

Marehemu atakumbukwa kwa kazi yake kubwa katika siasa za Tanzania ambapo amewahi kuwa mwanachama na kiongozi wa NCCR-Mageuzi, kabla ya kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM).