Tanzania yaialika China kuwekeza

0
2290

Mkutano wa Wakuu wa nchi na serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaanza Septemba Tatu jijini Beijing nchini China.

Katika mkutano huo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye tayari yuko nchini China anamuwakilisha Rais John Magufuli.

Akizungumza wakati wa mkutano wa wakuu wa kampuni na mashirika mbalimbali ya biashara jijini Beijing ikiwa ni maandalizi ya mkutano huo wa FOCAC, Waziri mkuu Kassim Majaliwa imeialika China kuwekeza katika ujenzi wa jiji la Dodoma hasa miundombinu pamoja na nyumba za watumishi .

Amesema kuwa ni wakati muafaka kwa kampuni kutoka nchini China kuwekeza katika maeneo mbalimbali ya Tanzania ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu na sekta ya madini.