Tanzania yafanya vizuri kwenye kilimo biashara

0
123

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi amesema Tanzania imeanza kufanya vizuri katika sekta ya Kilimo Biashara, hasa baada ya kuwa na mpango wa kuwawezesha Wanawake na Vijana katika kufanya shughuli hizo.

Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo mkoani Dar es Salaam ambapo mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika unaoendelea na kujumuisha wadau wa chakula kutoka Afrika na nje ya Bara hilo.

Amesema kumekuwa na ongezeko la Wanawake na Vijana kushiriki katika shughuli za Kilimo Biashara, jambo ambalo ni ishara ya mafanikio ya Tanzania katika kufikia malengo ya kuilisha Dunia.

Dkt. Mwinyi ameongeza kuwa pamoja na mafanikio yaliyoanza kuonekana bado kuna changamoto katika upatikanaji wa mitaji na teknolojia ya kisasa katika kufanya Kilimo Biashara.

“Mkutano huu unalenga kuhamasisha Mpango wa BBT ambao unalenga kuzalisha mazao ya chakula na mifugo na upatikanaji wa soko ya uhakika nje ya Tanzania ili Wanawake na Vijana wawe na taswira chanya kwenye Kilimo Biashara” Amesema Dkt. Mwinyi