Tanesco Dodoma yapewa siku 10 umeme kurejea katika hali yake

0
883

Waziri wa Nishati Dokta Merdan Kalemani ametoa Siku kumi na nne kwa Meneja wa Shirika la Umeme Mkoani Dodoma kuhakikisha umeme katika Jiji la Dodoma haukatiki mara kwa mara.

Dokta Kalemani amesema hayo katika ziara yake ya kukagua vituo vya kufulia umeme ambapo ameshuhudia umeme unaozalishwa ni mwingi na kuwepo na ziada na kutokuwepo kwa sababu ya umeme kukatikatika katika katika Jiji la Dodoma.

Pia amemtaka mkandarasi anayefanya upanuzi wa kituo cha kufulia umeme zuzu kukamilisha mradi  huo kwa wakati  ili kuhakikisha haujitokezi upungufu wa umeme kutokana na ongezeko la watumiaji wa umeme Mkoani Dodoma.

Katika hatua nyingine Waziri Kalemani amelitaka Shirika la Umeme Mkoani Dodoma kuimarisha ulinzi katika vituo vya kufulia umeme.