TALGWU Songwe waomba nyongeza ya mshahara

0
379

Katika kuadhimisha siku ya wafanyakazi Duniani katibu wa chama cha wafanyakazi wa serikali za mtaa(TALGWU) Mkoa wa Songwe Emanuel Alfonce ameiomba serikali kuwafikiria wafanyakazi katika ongezeko la mishahara

Aidha Alfonce ameongeza kuwa chama cha wafanyakazi kipo tayari kupinga rushwa makazini zinazokuwa sababu ya kurudisha nyuma jitihada za wafanyakazi kuwahudumia wananchi

Katika hatua nyingine Alfonce pia amesema chama hicho kipo tayari kushirikiana na serikali katika kuhakikisha zoezi zima la sensa ya watu na makazi linafanikiwa.