Shule kuunda madawati ya ulinzi wa mtoto

0
1131

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu amewataka wazee wanaoendeleza mila ya ukeketaji kutafuta njia mbadala ya kuwafundisha vijana bila kuwaumiza au kuathiri miili yao.

Akizungumza mkoani Mara wakati wa ufungaji kambi okozi mabinti zaidi ya 400 waliokimbia tohara mwaka 2018 na vijana 29 waliofanyiwa tohara salama katika kijiji cha Masanga wilayani Tarime, Dkt. Jingu amesema zipo njia za kuendeleza mila kwa kumfundisha binti mambo ya msingi ikiwemo elimu dunia.

Ameelezea mikakati ya serikali kulinda haki ya mama na mtoto ifikapo mwaka 2020 huku akitumia fursa hiyo kuwakumbusha walimu katika shule zote nchini kuunda madawati ya ulinzi wa mtoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la TGNP Lilian Liundi amesema ni muhimu jamii ikawa na usawa ili kufikia uchumi wa viwanda.