Shilingi Milioni Mia tatu zakusanywa kwa mwezi mmoja

0
2205

Zaidi ya shilingi milioni mia tatu zimekusanywa jijini Dar Es Salaam katika kipindi cha mwezi mmoja ikiwa ni faini kutoka kwa watu waliokutwa na makosa ya uchafuzi wa mazingira.

Akizungumza katika mkutano wa wadau wa usafi wa mazingira Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda amesema zoezi la usafi si la mkuu wa mkoa bali ni la kila mkazi wa jiji hilo.

Makonda amewaambia wadau wa usafi kwamba hali ya usafi imeimarika na kusema zaidi ya watu 11,000 wamepatikana na makosa yanayohusu uchafu wa mazingira.

Aidha wadau wa uzoaji taka wamekubali hoja ya kuzoa taka nyakati za usiku.