Shilingi Bilioni 8.6 kulipa fidia

0
2207

Serikali imetoa zaidi ya shilingi Bilioni 8.6 kulipa fidia wananchi wanaopisha upanuzi wa Ikulu ya Chamwino na Kiwanja cha Ndege cha Dodoma.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge katika mkutano na maafisa wa viwanja vya ndege na Wakala wa Majengo Nchini TBA.

Mkurugenzi Idara ya Miliki Wakala wa Majengo Nchini -TBA, Baltazari Kimanyamo amewahakikishia wakazi wa Chamwino kuwa hakuna atakaye chukuliwa ardhi yake bila kulipwa fidia.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini – TAA, Richard Mayongela amesema kuna changamoto katika kiwanja hicho cha ndege hali inayosababisha ndege kushindwa kutua nyakati za usiku mkoani Dodoma.