Serikali yataka ujenzi wa Rada kukamilika kwa wakati

0
938

Serikali imeitaka Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini -Tcaa kukamilisha kwa wakati ujenzi wa rada mpya ya kuongozea ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.

Agizo hilo limetolewa Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye baada ya kufanya ziara katika uwanja huo na kusema Rada hiyo inatakiwa ianze kutumika mapema kwa manufaa ya Taifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tcaa, Hamza johari ameahidi kutekeleza maagizo hayo.

Mkataba wa ujenzi wa Rada hiyo ulisainiwa March mwaka 2018 na ujenzi wake unatarajiwa kukamilika Septemba mwaka huu kwa gharama ya Shilingi Bilioni 67.3.