Serikali yataka kuharakishwa ujenzi barabara ya Tanga – Pangani

0
175

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa amesema Serikali ipo tayari kukamilisha malipo ya Mkandarasi wa ujenzi wa barabara ya Tanga – Pangani yenye urefu wa kilomita 50.

Waziri Mbarawa ametoa kauli hiyo baada ya kutembelea barabara hiyo inayojengwa kwa kiwango cha lami, ambapo ujenzi wake ulianza mwaka 2019 na kutakiwa kukamilika mwaka 2022.

Amesema fedha za kukamilisha ujenzi huo zipo tayari, kinachotakiwa ni kuongezeka kwa kasi ya ujenzi ili ikamilike na kuruhusu Wananchi kuitumia.

Katika hatua nyingine Serikali imetoa shilingi Bilioni nne kwa ajili ya kulipa fidia Wananchi 358 waliopitiwa na mradi huo wa barabara ya Tanga -:Pangani.

Hadi sasa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Tanga umelipa shilingi Bilioni 3.8, huku wengine wakiwa hawajalipwa kutokana na migogoro ya kifamilia.