Serikali yajipanga kutekeleza ahadi zake

0
2220

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema serikali ya awamu ya tano imejipanga kutekeleza ahadi zake na kuwatahadharisha wananchi kuwa macho na matapeli wanaopita vijijini kuchangisha fedha kwa madai ya kuwapa kipaumbele katika mgao wa shilingi milioni hamsini kwa kila kijiji.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Muzeze wilayani Buhigwe mkoani Kigoma.

Amesema fedha hizo hazijaanza kutolewa kutokana na kipaumbele kuelekezwa kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ya nchi.

Akiwa wilayani Buhigwe Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pia amezindua shamba la miti katika kijiji cha Muzeze na kuwataka watanzania kutunza mazingira.

Makamu wa Rais amehitimisha ziara yake ya siku nne mkoani Kigoma.