Serikali yafungua akaunti maafa Mv Nyerere

0
2139

Serikali imefungua akaunti maalum baada ya kivuko cha MV Nyerere kuzama Septemba 20 mwaka huu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama amesema watanzania wanaweza kutuma rambirambi zao katika akaunti hiyo itakayokuwa ikiratibiwa na ofisi ya maafa mkoa wa Mwanza chini ya usimamizi wa Ofisi ya maafa katika Ofisi ya Waziri Mkuu.

Akaunti hiyo ya maafa inaitwa Maafa MV Nyerere yenye namba 31110057246 katika Benki ya NMB tawi la Kenyatta Road mkoani Mwanza.

Waziri Mhagama amesema wale wote watakaoguswa kuchangia watume fedha katika akaunti hiyo.