Serikali yaendelea kutathmini mishahara bora

0
1811

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema serikali inaendelea na kazi ya kukamilisha tathmini katika Wizara na Taasisi ili kupanga vizuri mishahara na motisha kwa watumishi wa umma baada ya kumalizika kwa zoezi la kuwaondoa watumishi hewa.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jijini Dodoma baada ya kupokea maandamano ya wafanyakazi yaliyofanyika kwa lengo la kumpongeza Rais Magufuli kurudisha kikokotoo cha zamani katika mafao ya wastaafu.

“Serikali imeweka azma ya kuongeza motisha kwa wafanyakazi wote nchini ikiwemo na ulipaji wa madeni ya wafanyakazi”alisema Waziri Mkuu Majaliwa.