Serikali kuwarejesha Wafungwa wa kigeni nchini mwao

0
314

Serikali inafanya mazungumzo na Serikali ya Ethiopia ili kuona namna ya kuwarejesha nchini mwao Wahamiaji 1, 415 ambao wanatumikla kifungo katika magereza mbalimbali hapa nchini.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Sheria nchini, Siku inayoashiria kuanza kwa shughuli za Mahakama kwa mwaka huu.

Rais Magufuli amesema kuwa baada ya kukamilika kwa mazungumzo hayo, atasaini hati ya kuachiwa kwa Wafungwa hao raia wa kigeni ili waweze kurejea nchini mwao.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli, lengo la hatua hiyo ya Serikali ni kupunguza msongamano katika magereza mbalimbali hapa nchini.