Mkoa wa Dar es salaam watakiwa kuongeza kasi kukusanya kodi

0
1218

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amewataka wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa  manispaa na wakuu wa mamlaka ya mapato nchini kuangalia  uwezekano wa kuongeza makusanyo kutoka asilimia kumi na saba  hadi asilimia thelathini katika kipindi hiki cha mwaka 2019.

Akizungumza na viongozi hao katika kikao maalum cha utendaji ambacho kilikuwa kinapanga mkakati wa kuongeza  makusanyo ya mapato katika mkoa wa Dar es salaam ,Makonda  amesema lazima viongozi hao watambue fursa  nyingine za ukusanyaji wa mapato ili kuhakikisha yanaleta tija katika ustawi wa maendeleo ya mkoa wa Dar es salaam.

Pia amewataka viongozi hao kuwawezesha vijana kutambua fursa za ajira ambazo zitawawezesha vijana hao  kuondokana na umasikini.

Kikao hicho tendaji cha kupanga mkakati wa utafutaji wa fursa mbalimbali za makusanyajo wa mapato kimewashirikisha  wadau mbalimbali wakiwemo watendaji wakuu wa halmashauri,vikosi vya ulinzi na usalama ,maafisa kutoka idara mbalimbali na maafisa kutoka mamlaka ya mapato nchini –Tra.