Sakata la kutekwa kwa MO, watatu washikiliwa

0
2009

Watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam kufuatia tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara maarufu nchini Mohamed Dewji.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo, – Paul Makonda amesema kuwa vyombo vya ulinzi vinaendelea kumtafuta mfanyabiashara huyo na kuomba yeyote mwenye taarifa inayoweza kusaidia kupatikana kwake ashirikiane na jeshi la polisi.

Naye Kamanda wa polisi Kanda maalum ya Dar es salaam, –  Lazaro Mambosasa amesema kuwa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa kina wa tukio hilo na kusema kuwa kipaumbele kwa sasa ni kahakikisha Mohamed Dewji anapatikana akiwa salama.

Kwa mujibu wa Kamanda  Mambosasa, -Mohamed Dewji ametekwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni  raia wa kigeni.