Rais wa Ufaransa aandika barua ya wazi kwa raia wake

0
929

Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ameandika barua ya wazi kwa raia wa nchi hiyo ya kutaka kufanya mazungumzo  ya kitaifa  kutokana na maandamano yanayoendelea nchini humo.

Macron amewaandikia raia wake akisema anataka kuzigeuza hasira zao ziwe suluhisho.

Amesema mapendekezo yatakayotolewa katika mjadala huo yatasaidia kupanga vizuri kazi za serikali na bunge pamoja na nafasi ya Ufaransa barani na kimataifa.

Mada zitakazojadiliwa katika mazungumzo hayo ni kuhusiana na  kodi, demokrasia, ulinzi wa mazingira na uhamiaji.

Maandamano yajulikanayo  vizibao vya njano yamekuwa yakiendelea kwa wiki kadhaa sasa wakipinga sera za serikali ya  Macron.