Rais Samia: Lengo la Tamasha la Kizimkazi ni kurithisha utamaduni

0
168

Rais Samia Suluhu Hassan amesema lengo la Tamasha la Kizimkazi ni kurithisha utamaduni wa Kusini Unguja kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Akihutubia wakati wa hafla ya kilele cha Tamasha la Kizimkazi, Rais Samia amesema mbali na kurithisha utamaduni lakini pia lina lengo kuwaweka pamoja wananchi wa Kusini Unguja na kufurahi kwa pamoja.

“Wajukuu zetu hawajui hata vyakula vyetu wala tamaduni za huku. Tamasha hili lengo lake ni kuwakumbusha na kuwarithisha watoto na vizazi vyetu utamaduni wa watu wa Unguja Kusini,” amesema Rais Samia

Ameongeza kuwa mbali na mambo ya utamaduni lakini pia tamasha hilo limetumika kuzindua na kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kuvutia uwekezaji kwenye maeneo ya mkoa wa Kusini na Zanzibar kwa ujumla.

Miradi 12 imezinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi katika tamasha la mwaka huu ambapo Rais Samia ameshiriki.