Rais Magufuli atoa vitambulisho vya wajasiriamali

0
1649

Rais Dkt. John Magufuli ametoa vitambulisho 670,000 maalum kwa wajasiriamali wadogo nchini ambao wana biashara zenye mtaji usiozidi shilingi milioni nne na kusema kupitia vitambulisho hivyo hakuna mtu atakayewanyanyasa wafanyabiashara wadogo.

Rais Magufuli amekabidhi vitambulisho hivyo jijini Dar es Salaam kwa wakuu wa mikoa na kuonya wafanyabiashara kuacha kufanya shughuli zao katika sehemu zitakazosababisha usumbufu kwa wengine.

Vitambulisho hivyo vimetolewa katika mkutano maalum baina ya Rais Magufuli na uongozi wa Mamlaka ya Mapato Nchini – TRA ambapo vitambulisho hivyo vimetolewa na Ofisi ya Rais TAMISEMI na vitatumika kuanzia mwaka huu hadi mwaka 2019.