Rais Magufuli ateua wenyeviti wa taasisi tano za serikali

0
1971

Rais Dkt. John Magufuli ameteua wenyeviti wa bodi za taasisi tano za serikali baada ya wenyeviti waliokuwa wakiongoza bodi hizo kumaliza muda wao na wengine kuteuliwa katika nyadhifa nyingine.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, imesema walioteuliwa ni Profesa Charles Mkonyi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Mifupa (MOI), Mwamini Malemi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari, Sophia Simba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Magavana wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii, Dkt. Mwanza Kamata kuwa Mwenyekiti wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) na Dkt. Maria Mashingo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo (TIB).

Uteuzi wa wenyeviti hao wa bodi umeanza leo tarehe 22 Oktoba, 2018.