Rais Magufuli atangaza siku nne za maombolezo

0
2289

Rais Dkt. John Magufuli ametangaza siku nne za maombolezo kuanzia leo kufuatia vifo vya watu zaidi ya 130 vilivyotokana na kuzama kwa kivuko vya MV Nyerere.

Akihutubia taifa kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania –TBC, Rais Magufuli amewataka wanasiasa kutotumia msiba huu kupata umaarufu.

Rais Magufuli ametoa pole kwa watanzania wote hususan waliofiwa na ndugu na jamaa zao na kuwatakia majeruhi kupona haraka.

Aidha bendera zitapepea nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia kesho, Septemba 22 mwaka huu 2018.

Akizungumza jijini Dodoma kwa niaba ya Rais Dkt. Magufuli, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi ameagiza watu wote wanaohusika na shughuli za uendeshaji wa kivuko cha MV Nyerere kukamatwa na kuhojiwa na watakaokutwa na hatia wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.