Rais Magufuli ataka taasisi za umma kuunganishwa mfumo wa elektroniki

0
1081

Rais Dkt. John Magufuli ameagiza Taasisi za Umma kuunganishwa kwenye mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki ili kuiwezesha serikali kufahamu kiwango cha mapato kutoka kwenye taasisi hizo na kutumika kwa maendeleo ya taifa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo jijini Dar Es Salaam wakati akizindua mfumo mpya wa kusimamia uwazi katika mawasiliano ya simu (TTMS) ambapo amesema tangu mfumo huo uanze serikali imekusanya shilingi Bilioni 93.6.

Pia Rais Magufuli amewapongeza watumishi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania –TCRA kwa kuchapa kazi bila woga kwa kutanguliza maslahi ya taifa mbele.

Halikadhalika Rais Magufuli ameongeza mkataba wa miaka mitano wa utumishi kwa Mkurugunzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba amesema kukamilika kwa mradi huo, kutachochea ukusanyaji wa mapato kupitia miamala ya fedha kwa njia ya mawasiliano.