Rais Magufuli apokea hati za utambulisho za mabalozi

0
1932

 

Rais John Magufuli kwa nyakati tofauti hii leo amepokea hati za utambulisho za mabalozi wapya watano wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Hafla ya kupokea hati hizo za mabalozi wapya wa Ubelgiji, Norway, Sweden, Palestina na Kuwait imefanyika Ikulu jijini Dar es salaam.

Mara baada ya Rais Magufuli kupokea hati hizo za utambulisho, alifanya mazungumzo na mabalozi hao wapya kwa nyakati tofauti, mazungumzo yalioyohusu masuala ya kiuchumi na kisiasa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustine Mahiga ambaye naye ameshuhudia mazungumzo hayo amesema kuwa Rais Magufuli na mabalozi hao wapya wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wamesisitiza kudumishwa kwa uhusiano na ushirikiano baina ya Tanzania na mataifa hayo.