Rais Magufuli akutana na Dkt Kikwete

0
1899

Rais John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete  Ikulu jijini Dar es salaam.

Baada ya mazungumzo yao, Rais Mstaafu Kikwete amesema kuwa wamekutana kwa utaratibu wa kawaida wa kusalimiana na kutakiana heri katika majukumu.

Aidha, Rais Mstaafu Kikwete amebainisha kuwa Rais Magufuli anafanya kazi nzuri na amemtaka aendelee hivyo hivyo.

Nimekuja kumsalimia na kumtakia kila la heri, anafanya kazi nzuri, aendelee tu kuchapa kazi na sisi tupo kwa namna yoyote ya kumpa nguvu, tupo tayari kumsaidiaamesema Rais Mstaafu Kikwete.