Rais Magufuli afanya uteuzi

0
2276

Rais John Magufuli amemteua Dkt John Jingu kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Kabla ya uteuzi huo Dkt Jingu alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais – Ikulu imesema kuwa Dkt Jingu anachukua nafasi ya Sihaba Nkinga ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Wakati huohuo Rais Magufuli amemteua Gabriel Malata kuwa Kamishna wa Kazi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.

Kabla ya uteuzi huo Malata alikuwa Mkurugenzi Msaidizi Kesi za Madai, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Malata anachukua nafasi ya Hilda Kabisa ambaye uteuzi wake umetenguliwa.