Rais Magufuli afanya uteuzi

0
2268

Rais Dkt. John Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali wa taasisi za umma.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema walioteuliwa ni  Pius Msekwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya na Zakia Meghji kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho.

Halikadhalika Rais Magufuli amemteua Profesa Esnati Chaggu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira –NEMC, Dkt. Samwel Gwamaka kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC.

Wengine walioteuliwa ni Meja Jenerali Mstaafu Michael Isamuhyo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa –STAMICO, Profesa Gaspar Mhinzi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli – PURA.

Uteuzi wa viongozi hawa umeanza leo tarehe 06 Desemba, 2018.