Rais Magufuli afanya teuzi

0
1724

Rais Dkt. John Magufuli amemteua Balozi Luteni Jenerali Mstaafu Wyjones Kisamba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumbu.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema Balozi Kisamba anachukua nafasi ya Profesa Burton Mwamila ambaye amemaliza muda wake.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Mbaraka Semwanza kuwa Kamishna wa Utawala na Fedha katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Semwanza anachukua nafasi ya Michael Shija ambaye amestaafu.

Uteuzi wa viongozi hao umeanza leo.