Necta yawafutia matokeo wanafunzi 47 wa kidato cha pili

0
1359

Baraza la Mitihani nchini -Necta limewafutia matokeo jumla ya wanafunzi 47 wa Kidato cha Pili na 151 wa darasa la nne kwa kufanya udanganyifu na kuandika lugha ya matusi katika mitahani yao.

Akitangaza matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili na Darasa la nne kwa 2018 Katibu mtendaji wa necta Dokta Charles Msonde Jijini Dodoma amesema kiwango cha ufaulu kimeongezeka ikilinganishwa na mwaka 2017.

Dokta Msonde kwanza akaweka wazi kiwango cha ufaulu katika matokeo ya mtihani wa Kidato cha Pili kwa mwaka 2018.

Pia akaitaja mikoa mikoa iliyofanya vizuri na mikoa iliyofanya vibaya katika Mitihani ya kidato cha pili kitaifa.

Katika matokeo ya Kidato cha pili wasichana wameongoza kwa ufaulu ambapo katika kumi bora wasichana wako saba kati ya kumi huku nafasi ya kwanza hadi ya sita kitaifa ikishikiliwa na wasichana.