Mwili wa Meja Jenerali Mstaafu Lesulie waagwa

0
2818

Rais John Magufuli ameongoza waombolezaji kuuaga mwili wa Meja Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Joseph Anael Lesulie aliyefariki dunia Agosti 14 mwaka huu katika hospitali ya taifa ya muhimbili jijini Dar es salaa alikokuwa akipatiwa matibabu.

Shughuli ya kuuaga mwili wa meja jenerali mstaafu lesulie imefanyika nyumbani kwa marehemu katika eneo la ada estate, kinondoni jijini Dar es salaam.

Meja Jenerali Mstaafu Lesulie anazikwa hii leo katika makaburi ya kinondoni jijini dar es salaam.