Mwili wa kada wa CCM aliyepotea waokotwa Njombe

0
952

Jeshi la Polisi mkoani Njombe limethibitisha kuokotwa kwa mwili wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa, Emmanuel Polycarp Mlelwa aliyekuwa amepotea katika mazingira ya kutatanisha.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Njombe, Hamisi Issa ameiambia TBC kuwa jeshi la polisi mkoani humo linaendelea na uchunguzi na litaendele kutoa taarifa kuhusiana na tukio hilo.

Mlelwa alikuwa mwenyekiti wa seneti ya wananfunzi wa vyuo na vyuo vikuu wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa na mwili wake umekotwa katika eneo la Kibena Bwawani.