Mtihani wa kidato cha pili Zanzibar wafutwa

0
1699

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imefuta mtihani wa kidato cha Pili ulioanza leo baada ya kubaini udanganyifu uliosababisha kuvuja kwa mitihani hiyo.

Waziri wa Elimu Zanzibar Riziki Pembe Juma amesema wizara imefikia uamuzi huo kufuatia taarifa za kuaminika za kuvujishwa kwa baadhi ya mitihani ya kidato cha Pili na tayari baadhi ya wahusika wameanza kushikiliwa na vyombo vya dola.

Amesema kutokana na udanganyifu huo serikali imeingia hasara ya zaidi ya shilingi milioni 250 na kwamba tarehe ya kufanyika tena kwa mtihani wa kidato cha Pili itatangazwa hapo baadae.