Msigwa : Tanzania haina Wafungwa wa kisiasa

0
375

Serikali imetaka kupuuzwa kwa taarifa zinazosambazwa mitandaoni na katika chombo cha habari kutoka nchi jirani ya Kenya zinazosema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameachia wafungwa wa kisiasa.

Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa amesema Rais Samia Suluhu Hassan hawezi kuingilia mahakama na kwamba Tanzania haina wafungwa wa kisiasa.

Amesema kuwa hatua mbalimbali za kisheria zinafuatwa, kufuatia usambazwaji wa taarifa hizo za uongo.