Msemaji wa familia aeleza sababu za kifo cha Mzee Mkapa

0
132

Siku tatu za kuuaga mwili wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa zimeanza rasmi leo katika Uwanja wa Uhuru, Dar es salaam.

Zoezi hili la kuuaga mwili wa marehemu Mkapa limeanza kwa misa takatifu na litaendelea hadi Jumanne tarehe 28 Julai 2020.

Aidha, msemaji wa familia, William Erio ameeleza kuwa Hayati Mkapa alifariki dunia kutokana na mshituko wa moyo.

Mwili wa Mzee Mkapa umehifadhiwa katika eneo maalum tayari kwa wananchi kutoa heshima za mwisho.