Msangi aitembelea TBC

0
1626

Jeshi la Polisi Nchini limejipanga kudhibiti vitendo vya uhalifu katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka za Krismasi na Mwaka Mpya na kuwaomba Watanzania wote kushirikiana na Jeshi hilo ili kuwafichua  wahalifu kwenye maeneo mbalimbali.

Kauli hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini, – Ahmed Msangi alipofanya ziara ya kutembelea ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) eneo la Mikocheni jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa Jeshi hilo lipo imara katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu.

Kwa mujibu wa Kamanda Msangi, kufuatia elimu ya usalama barabarani inayotolewa na Jeshi hilo mara kwa mara,  ajali za barabarani zimepungua kwa kiasi kikubwa kuanzia mwezi Januari hadi Oktoba mwaka huu na kutaka kuzingatiwa kwa sheria za usalama barabarani kipindi hiki cha kuelekea Sikukuu za mwisho wa mwaka .

Ziara hiyo ya Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini katika Shirika la Utangazaji Tanzania, ilikua na lengo la kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni.