Mkutano wa 12 wa Bunge waanza

0
2148

Mkutano wa Kumi na Mbili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano umeanza kwa Spika wa Bunge Job Ndugai kumuapisha Mhandisi Christopher Chizza ambaye ni Mbunge wa jimbo la Buyungu mkoani Kigoma aliyechaguliwa katika uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika Agosti 12 mwaka 2018.

Shughuli nyingine itakayofanyika kwenye mkutano huo utakaomalizika Septemba 14 ni kupitisha kwa hatua zilizobaki miswada Mitano ya sheria ambayo ilisomwa kwa mara ya kwanza katika mkutano wa Kumi na Moja Bunge.

Maswali 125 ya kawaida yataulizwa na mengine 16 ya papo kwa papo yataulizwa kwa Waziri Mkuu wakati wa mkutano huo wa 12 wa Bunge.